Ecclesiastes 11:7-10

Mkumbuke Muumba Wako Ukiwa Bado Kijana


7 aNuru ni tamu,
tena inafurahisha macho kuona jua.

8 Hata kama mtu ataishi miaka mingi kiasi gani,
na aifurahie yote.
Lakini na akumbuke siku za giza,
kwa maana zitakuwa nyingi.
Kila kitu kitakachokuja ni ubatili.


9 bFurahi ewe kijana, wakati ungali kijana,
moyo wako na ukupe furaha
katika siku za ujana wako.
Fuata njia za moyo wako
na chochote macho yako yaonayo,
lakini ujue kwamba kwa ajili ya haya yote
Mungu atakuleta hukumuni.

10 cKwa hiyo basi, ondoa wasiwasi moyoni mwako
na utupilie mbali masumbufu ya mwili wako,
kwa kuwa ujana na nguvu ni ubatili.
Copyright information for SwhKC